Psalms 98:1-6
Mungu Mtawala Wa Dunia
(Zaburi)
1 aMwimbieni Bwana wimbo mpya,
kwa maana ametenda mambo ya ajabu;
kitanga chake cha kuume na mkono wake mtakatifu
umemfanyia wokovu.
2 b Bwana ameufanya wokovu wake ujulikane
na amedhihirisha haki yake kwa mataifa.
3 cAmeukumbuka upendo wake
na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli;
miisho yote ya dunia imeuona
wokovu wa Mungu wetu.
4 dMpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote,
ipaze sauti kwa nyimbo za shangwe na vinanda;
5 emwimbieni Bwana kwa kinubi,
kwa kinubi na sauti za kuimba,
6 fkwa tarumbeta na mvumo wa baragumu za pembe za kondoo dume:
shangilieni kwa furaha mbele za Bwana, aliye Mfalme.
Copyright information for
SwhKC